AGIZO la mwaka 2021 la Rais, Samia Suluhu Hassan, la kuruhusu wanafunzi waliokatisha masomo, wakiwemo waliopata ujauzito, kurejea na kuendelea na elimu, limeanza kuzaa matunda. Maendeleo hayo yanaonekana kupitia Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi (FDC) ambavyo vinasaidia kuwajengea wanafunzi hao upya ndoto zao na kuwawezesha kujitegemea.

Hali hiyo imebainika kufuatia ziara ya Daily News Digital na Habari Leo katika vyuo vya FDC wilayani Urambo na Sikonge, mkoani Tabora. Katika ziara hiyo, wanafunzi wanaosomea masomo ya QT na fani mbalimbali za ufundi walionekana kurejea darasani kwa ari mpya, wakionesha matumaini ya kujikwamua kiuchumi kupitia elimu wanayoipata. SOMA: Wanafunzi 18 watua Korea kimasomo