Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araqchi amewasili St. Petersburg, Urusi ambapo anatarajiwa kukutana na Rais wa Urusi Vladimir Putin mjini Moscow, shirika la habari la Iran, limeripoti likimnukuu balozi wa Iran nchini Urusi, Kazem Jalali.

Bwana Araghchi alisafiri kwa ndege ya "Minab Flight 168" kuwakumbuka watoto waliouawa katika shule ya Minab, Mkoa wa Hormozgan, waliouawa katika shambulio la Marekani na Israel dhidi ya Iran.

Madhumuni ya ziara ya Bw. Araqchi inaelezwa kuwa "kukutana na kujadiliana na Rais wa Urusi Vladimir Putin."

Siku ya Jumapili, baada ya kusafiri hadi Muscat na kukutana na maafisa wa Oman, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran alielekea Islamabad kwa mara ya pili katika siku tatu zilizopita, na kukutana na maafisa wa Pakistan kabla ya kuondoka kwenda Moscow.

Maelezo ya ziara hizi na sababu ya kurejea kwake Oman na Pakistan bado haijafichuliwa