Idadi ya meli za kubeba mafuta zinazopita kila siku katika Mlango Bahari wa Hormuz imeonekana kupungua hii leo siku ya Ijumaa, baada ya Marekani na Iran kushambuliana na kuendeleza mabishano kuhusu nani anayedhibiti njia hiyo muhimu ya baharini.
Mashambulizi hayo yamezua tena wasiwasi kuhusu kuimarika kwa shughuli za usambazaji wa mafuta duniani na usafirishaji kwa njia ya bahari.
Hali hii inaonyesha jinsi makubaliano ya muda ya kusitisha mapigano yalivyo dhaifu huku Marekani na Iran zikiendelea kujadiliana ili kufikia makubaliano ya kudumu.
0 Comments