Korea Kusini imesema mazoezi yake ya pamoja ya kijeshi na Marekani yatamalizika siku sita kabla ya muda uliopangwa, huku pia yakipunguzwa kwa kiwango.

Hatua hiyo inafuatia agizo la Rais wa Marekani Donald Trump la kupunguza mazoezi hayo, akisema hayafai na yanaweza kuchukuliwa kuwa ya uchokozi dhidi ya Korea Kaskazini.

Ripoti ambazo hazijathibitishwa zinaeleza kuwa Trump anatarajia kukutana na kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong Un, baadaye mwaka huu.

Rais wa Korea Kusini, Lee Jae Myung, amesema nchi yake inahitaji kujenga uwezo imara na huru wa kijeshi, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kupunguza utegemezi wake kwa Marekani katika masuala ya ulinzi.